بسم الله الرحمن الرحيم

نتائج البحث: 6236
ترتيب الآيةرقم السورةرقم الآيةالاية
278223109إنه كان فريق من عبادي يقولون ربنا آمنا فاغفر لنا وارحمنا وأنت خير الراحمين
Bila ya shaka lilikuwapo kundi katika waja wangu likisema: Mola wetu Mlezi! Tumeamini; basi tusamehe na uturehemu, nawe ndiwe Mbora wa wanao rehemu.
278323110فاتخذتموهم سخريا حتى أنسوكم ذكري وكنتم منهم تضحكون
Lakini nyinyi mliwakejeli hata wakakusahaulisheni kunikumbuka, na mlikuwa mkiwacheka.
278423111إني جزيتهم اليوم بما صبروا أنهم هم الفائزون
Hakika Mimi leo nimewalipa kwa vile walivyo subiri. Bila ya shaka hao ndio wenye kufuzu.
278523112قال كم لبثتم في الأرض عدد سنين
Atasema: Mlikaa muda gani katika ardhi kwa hisabu ya miaka?
278623113قالوا لبثنا يوما أو بعض يوم فاسأل العادين
Watasema: Tulikaa siku moja au sehemu ya siku. Basi waulize wanao weka hisabu.
278723114قال إن لبثتم إلا قليلا لو أنكم كنتم تعلمون
Atasema: Nyinyi hamkukaa huko duniani ila kidogo, laiti ingeli kuwa mnajua.
278823115أفحسبتم أنما خلقناكم عبثا وأنكم إلينا لا ترجعون
Je! Mlidhani ya kwamba tulikuumbeni bure na ya kwamba nyinyi kwetu hamtarudishwa?
278923116فتعالى الله الملك الحق لا إله إلا هو رب العرش الكريم
Ametukuka Mwenyezi Mungu, Mfalme wa Haki, hapana mungu ila Yeye, Mola Mlezi wa A'rshi Tukufu.
279023117ومن يدع مع الله إلها آخر لا برهان له به فإنما حسابه عند ربه إنه لا يفلح الكافرون
Na anaye muomba - pamoja na Mwenyezi Mungu - mungu mwenginewe hana ushahidi wa hili; basi bila ya shaka hisabu yake iko kwa Mola wake Mlezi. Kwa hakika makafiri hawafanikiwi.
279123118وقل رب اغفر وارحم وأنت خير الراحمين
Nawe sema: Mola wangu Mlezi! Samehe na urehemu nawe ni Mbora wa wanao rehemu.


0 ... 268.1 269.1 270.1 271.1 272.1 273.1 274.1 275.1 276.1 277.1 279.1 280.1 281.1 282.1 283.1 284.1 285.1 286.1 287.1 ... 623

إنتاج هذه المادة أخد: 0.02 ثانية


المغرب.كووم © ٢٠٠٩ - ١٤٣٠ © الحـمـد لله الـذي سـخـر لـنا هـذا :: وقف لله تعالى وصدقة جارية

25393021454637512414705373433755811958