بسم الله الرحمن الرحيم

نتائج البحث: 6236
ترتيب الآيةرقم السورةرقم الآيةالاية
27142341فأخذتهم الصيحة بالحق فجعلناهم غثاء فبعدا للقوم الظالمين
Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhaalimu!
27152342ثم أنشأنا من بعدهم قرونا آخرين
Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine.
27162343ما تسبق من أمة أجلها وما يستأخرون
Hapana umma uwezao kutanguliza ajali yake wala kuikawiza.
27172344ثم أرسلنا رسلنا تترى كل ما جاء أمة رسولها كذبوه فأتبعنا بعضهم بعضا وجعلناهم أحاديث فبعدا لقوم لا يؤمنون
Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafuatanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini.
27182345ثم أرسلنا موسى وأخاه هارون بآياتنا وسلطان مبين
Kisha tukamtuma Musa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi.
27192346إلى فرعون وملئه فاستكبروا وكانوا قوما عالين
Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri.
27202347فقالوا أنؤمن لبشرين مثلنا وقومهما لنا عابدون
Wakasema: Je, tuwaamini wanaadamu wawili hawa kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?
27212348فكذبوهما فكانوا من المهلكين
Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa.
27222349ولقد آتينا موسى الكتاب لعلهم يهتدون
Na hakika tulimpa Musa Kitabu ili wapate kuongoka.
27232350وجعلنا ابن مريم وأمه آية وآويناهما إلى ربوة ذات قرار ومعين
Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji.


0 ... 261.3 262.3 263.3 264.3 265.3 266.3 267.3 268.3 269.3 270.3 272.3 273.3 274.3 275.3 276.3 277.3 278.3 279.3 280.3 ... 623

إنتاج هذه المادة أخد: 0.02 ثانية


المغرب.كووم © ٢٠٠٩ - ١٤٣٠ © الحـمـد لله الـذي سـخـر لـنا هـذا :: وقف لله تعالى وصدقة جارية

436226075873567118144051865236013385876