بسم الله الرحمن الرحيم

نتائج البحث: 6236
ترتيب الآيةرقم السورةرقم الآيةالاية
27012328فإذا استويت أنت ومن معك على الفلك فقل الحمد لله الذي نجانا من القوم الظالمين
Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu, aliye tuokoa na watu madhaalimu!
27022329وقل رب أنزلني منزلا مباركا وأنت خير المنزلين
Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji.
27032330إن في ذلك لآيات وإن كنا لمبتلين
Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani.
27042331ثم أنشأنا من بعدهم قرنا آخرين
Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine.
27052332فأرسلنا فيهم رسولا منهم أن اعبدوا الله ما لكم من إله غيره أفلا تتقون
Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Mwenyezi Mungu! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamwogopi?
27062333وقال الملأ من قومه الذين كفروا وكذبوا بلقاء الآخرة وأترفناهم في الحياة الدنيا ما هذا إلا بشر مثلكم يأكل مما تأكلون منه ويشرب مما تشربون
Na wakubwa katika watu wake walio kufuru na wakakanusha mkutano wa Akhera, na tukawadekeza kwa starehe katika maisha ya dunia, walisema: Huyu si chochote ila ni binaadamu kama nyinyi; anakula mlacho, na anakunywa mnywacho.
27072334ولئن أطعتم بشرا مثلكم إنكم إذا لخاسرون
Na nyinyi mkimt'ii mtu kama nyinyi basi hakika mtakuwa khasarani.
27082335أيعدكم أنكم إذا متم وكنتم ترابا وعظاما أنكم مخرجون
Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?
27092336هيهات هيهات لما توعدون
Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa.
27102337إن هي إلا حياتنا الدنيا نموت ونحيا وما نحن بمبعوثين
Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa.


0 ... 260 261 262 263 264 265 266 267 268 269 271 272 273 274 275 276 277 278 279 ... 623

إنتاج هذه المادة أخد: 0.02 ثانية


المغرب.كووم © ٢٠٠٩ - ١٤٣٠ © الحـمـد لله الـذي سـخـر لـنا هـذا :: وقف لله تعالى وصدقة جارية

105532469001518301814224408125932395906