بسم الله الرحمن الرحيم

نتائج البحث: 6236
ترتيب الآيةرقم السورةرقم الآيةالاية
23942046قال لا تخافا إنني معكما أسمع وأرى
Akasema: Msiogope! Hakika Mimi ni pamoja nanyi. Nasikia na ninaona.
23952047فأتياه فقولا إنا رسولا ربك فأرسل معنا بني إسرائيل ولا تعذبهم قد جئناك بآية من ربك والسلام على من اتبع الهدى
Basi mwendeeni, na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola wako Mlezi! Basi waache Wana wa Israili watoke nasi, wala usiwaadhibu. Sisi tumekuletea ishara itokayo kwa Mola wako Mlezi. Na amani itakuwa juu ya aliye fuata uwongofu.
23962048إنا قد أوحي إلينا أن العذاب على من كذب وتولى
Hakika tumefunuliwa sisi kwamba hapana shaka adhabu itamsibu anaye kadhibisha na akapuuza.
23972049قال فمن ربكما يا موسى
(Firauni) akasema: Basi Mola wenu Mlezi ni nani, ewe Musa?
23982050قال ربنا الذي أعطى كل شيء خلقه ثم هدى
Akasema: Mola wetu Mlezi ni yule aliye kipa kila kitu umbo lake, kisha akakiongoa.
23992051قال فما بال القرون الأولى
Akasema: Nini hali ya karne za kwanza?
24002052قال علمها عند ربي في كتاب لا يضل ربي ولا ينسى
Akasema: Ilimu yake iko kwa Mola wangu Mlezi katika Kitabu. Mola wangu Mlezi hapotei wala hasahau.
24012053الذي جعل لكم الأرض مهدا وسلك لكم فيها سبلا وأنزل من السماء ماء فأخرجنا به أزواجا من نبات شتى
Ambaye amekufanyieni ardhi kuwa tandiko, na akakupitishieni humo njia, na akakuteremshieni kutoka mbinguni maji. Na kwa hayo tukatoa namna mbali mbali za mimema.
24022054كلوا وارعوا أنعامكم إن في ذلك لآيات لأولي النهى
Kuleni, na mchunge wanyama wenu. Hakika katika hayo zipo ishara kwa wenye akili.
24032055منها خلقناكم وفيها نعيدكم ومنها نخرجكم تارة أخرى
Kutokana nayo (ardhi) tumekuumbeni, na humo tunakurudisheni, na kutoka humo tutakutoeni mara nyengine.


0 ... 229.3 230.3 231.3 232.3 233.3 234.3 235.3 236.3 237.3 238.3 240.3 241.3 242.3 243.3 244.3 245.3 246.3 247.3 248.3 ... 623

إنتاج هذه المادة أخد: 0.02 ثانية


المغرب.كووم © ٢٠٠٩ - ١٤٣٠ © الحـمـد لله الـذي سـخـر لـنا هـذا :: وقف لله تعالى وصدقة جارية

622410149871285311639031988584412141707