بسم الله الرحمن الرحيم

نتائج البحث: 6236
ترتيب الآيةرقم السورةرقم الآيةالاية
22741924فناداها من تحتها ألا تحزني قد جعل ربك تحتك سريا
Pakatangazwa kutoka chini yake: Usihuzunike! Hakika Mola wako Mlezi amejaalia chini yako kijito kidogo cha maji!
22751925وهزي إليك بجذع النخلة تساقط عليك رطبا جنيا
Na litikise kwako hilo shina la mtende, utakuangushia tende nzuri zilizo mbivu.
22761926فكلي واشربي وقري عينا فإما ترين من البشر أحدا فقولي إني نذرت للرحمن صوما فلن أكلم اليوم إنسيا
Basi kula, na kunywa, na litue jicho lako. Na pindi ukimwona mtu yeyote basi sema: Hakika mimi nimeweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga; kwa hivyo leo sitasema na mtu.
22771927فأتت به قومها تحمله قالوا يا مريم لقد جئت شيئا فريا
Akenda naye (mwanawe) kwa jamaa zake amembeba. Wakasema: Ewe Maryamu! Hakika umeleta kitu cha ajabu!
22781928يا أخت هارون ما كان أبوك امرأ سوء وما كانت أمك بغيا
Ewe dada yake Harun! Baba yako hakuwa mtu muovu, wala mama yako hakuwa kahaba.
22791929فأشارت إليه قالوا كيف نكلم من كان في المهد صبيا
Akawaashiria (mtoto). Wakasema: Vipi tumsemeze aliye bado mdogo yumo katika mlezi?
22801930قال إني عبد الله آتاني الكتاب وجعلني نبيا
(Mtoto) akasema: Hakika mimi ni mtumwa wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu, na amenifanya Nabii.
22811931وجعلني مباركا أين ما كنت وأوصاني بالصلاة والزكاة ما دمت حيا
Na amenijaalia ni mwenye kubarikiwa popote pale niwapo. Na ameniusia Sala na Zaka maadamu ni hai,
22821932وبرا بوالدتي ولم يجعلني جبارا شقيا
Na nimtendee wema mama yangu. Wala hakunifanya niwe jeuri, mwovu.
22831933والسلام علي يوم ولدت ويوم أموت ويوم أبعث حيا
Na amani iko juu yangu siku niliyo zaliwa, na siku nitakayo kufa, na siku nitakayo fufuliwa kuwa hai.


0 ... 217.3 218.3 219.3 220.3 221.3 222.3 223.3 224.3 225.3 226.3 228.3 229.3 230.3 231.3 232.3 233.3 234.3 235.3 236.3 ... 623

إنتاج هذه المادة أخد: 0.02 ثانية


المغرب.كووم © ٢٠٠٩ - ١٤٣٠ © الحـمـد لله الـذي سـخـر لـنا هـذا :: وقف لله تعالى وصدقة جارية

5067485338420476084211972651839012860